Wednesday, February 29, 2012

KAMA KESHO UMEINGIA CHUMBANI KUFANYA NINI?


MZEE wa Chabo kama kawaida yake baada ya kazi alikiwa anarejea nyumbani kupitia njia ya kichochoroni alisikia mabishano kati ya mwanamke na mwanaume ambapo mwanaume alisema:

“Sasa itakuwaje?”
“Si nimekueleza kesho leo hapana.”
Mzee wa Chabo alirudi hadi kwenye dirisha, aliweza kuwaona mwanamke na mwanaume wamekaa kitandani kimahaba.
“Acha hizo si ulikubali kuwa unanipa sasa tatizo nini?” 

“Nina wasiwasi mume wangu yupo njiani anarudi.”
“Huu muda tunaobishana si ningekuwa nimemaliza.”
“Hapana kesho bwana,” mwanamke aligoma.

Mzee wa Chabo alijikuta akikasilika japo shughuli haikuwa yake alijikuta akipayuka kwa hasira.
“Wanawake wengine washamba, sasa kama kesho umeingia chumbani kufanya nini?”



Courtesy : The Globalpublishers