Saturday, March 3, 2012

SITI YA DEREVA


Wakati watu wanagombania kupanda kwenye basi la kwenda Mbagala kama kawaida yao, bibi mmoja alipanda bila shida akapata siti na kukaa. Baada ya muda konda alimuuliza bibi:

Konda: Bibi unalia nini?’

Bibi alijibu huku akifuta machozi kwa upande wa khanga: Miaka yote 25 niliyoishi Mbagala leo ndiyo nimebahatika kupata siti.

Konda alimshangaa na kumwambia: Samahani bibi siti uliyokalia ni ya dereva.




Courtesy : The GlobalPublishers